Matapeli wa madini
Magenge ya matapeli kwenye biashara ya madini, yameibuka na kuendesha shughuli zake bila hofu. Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI umebaini kuwapo kwa matukio ya utapeli na kuifanya sifa ya Tanzania izidi kuchafuka mbele ya jumuiya ya kimataifa. Mwaka 2013, JAMHURI lilichapisha majina na kampuni za matapeli wa madini; hatua iliyoifanya Serikali ikunjue makucha kupambana na magenge…