November 2017
Zaidi ya Million 20 Zapatikana Kusaidia Watoto Wenye Ulemavu
Zaidi ya milioni 20 zimetolewa na wananchi pamoja na Taasisi mbalimbali hapa nchini ikiwa ni mchango wa kusaidia matibabu na kununua vifaa tiba kwa ajili ya watoto wenye vichwa vikubwa na migongo wazi. Ikiwa Jana ni Jumanne ya kutoa (GIVING TUESDAY) kote duniani na Taasisi ya Foundation for Civil Society iliadhimisha kwa kuwasaidia watoto hawa…
LHRC Yabaini Mapungufu Kibao Uchaguzi wa Madiwani
MKURUGENZI wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Anna Henga, amesema kuwa kituo hicho kimefuatilia kwa ukaribu uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43 ulifanyika Novemba 26 mwaka huu, katika halmashauri 36 kwenye mikoa 19 nchini. Katika uchaguzi huo tume ya haki za binadamu imebaini matukio mbalimbali ya uvunjifu mkubwa wa haki…
Katibu wa CHADEMA Manyara Arejea CCM
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Simanjiro, Mkoa wa Manyara, Meshack Turento ametangaza kujivua wadhifa huo na kujiunga na Chama cha Mapinduzi akidai chama hicho (CHADEMA) imewatelekeza. Akizungumza jijini Arusha Turento alidai kuwa, kabla ya kujiunga na CHADEMA alikuwa mwanachama wa CCM, lakini baadae aliona chama hicho kimepoteza mwelekeo na kujiunga…
Samia Suluhu Amtembelea Tundu Lissu Nairobi Hospital
MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan leo Jumanne Novemba 28, 2017 amemtembelea na kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu aliyelazwa Hospitali ya Nairobi. Samia amtembelea Lissu baada ya kumalizika kwa hafla ya kumwapisha Rais Uhuru Kenyatta kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya katika uwanja wa Moi Kasarani Mjini Nairobi. Mhe. Samia Suluhu…
MAJALIWA: Tutawashughulikia Wote Wanaotumia Vibaya Fedha Za Ukimwi
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haitawavumilia watu wote wanaotumia vibaya fedha za umma ambazo zinapaswa kuleta maendeleo kwa wananchi, zikiwemo na za Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi. Amesema mfuko huo unalenga kufanikisha ukusanyaji wa fedha za kutosha amabazo ni muhimu kwa Taifa wakati huu tunapoazimia kumaliza ukimwi ifikapo mwaka 2030.. Waziri Mkuu alitoa…