Matokeo ya Uchaguzi Siha Kutoka Vituo Mbalimbali
MATOKEO ya awali ya uchaguzi wa ubunge Jimbo la Siha yameanza kubandikwa nje ya vituo vya kupigia kura yakionyesha mgombea wa CCM, Dk Godwin Mollel akiongoza kwa mbali katika baadhi ya vituo. Katika matokeo hayo, Dk Mollel anafuatiwa kwa mbali na mgombea wa Chadema, Alvis Mossi huku wa CUF, Tumsifuel Mwanri akishika nafasi ya tatu…