Simba Yazidi Kuukaribia Ubingwa, Yaikung’uta Mtibwa Sugar Bao 1-0
Simba SC imeendelea kujikita kileleni katika Ligi Kuu Bara baada ya kuitandika Mtibwa Sugar bao 1-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. Mchezo huo uliokuwa unaambatana na mvua iliyokuwa ikinyesha Uwanjani, ulishuhudiwa nyavu zikitikiswa mnamo dakika ya 24 ya kipindi cha kwanza na Emmanuel Okwi. Okwi alifunga bao hilo akimalizia kazi mpira wa kichwa kutoka…