Maandiko ya Mwalimu Nyerere: Ujamaa Sehemu ya 3
Leo Tanganyika ni nchi masikini. Hali ya maisha ya umma iko chini kiasi cha kuaibisha. Lakini kama kila mtu katika nchi, mke kwa mume, atatambua hayo na kufanya kazi ukomo wa nguvu zake, kwa faida ya nchi nzima, basi Tanganyika itaendelea; na maendeleo hayo kila mtu atayapata. Lakini mafanikio haya lazima yagawanywe kwa watu wote….