Tangazo la NEC lahitimisha udiwani wa Manji
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata 21 ikiwamo ya Mbagala Kuu katika Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam, jambo linalohitimisha udiwani wa mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Athuman Kihamia, juzi alitangaza uchaguzi huo mdogo kupitia taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari. Katika taarifa…