Mahakama yamuachia huru mbunge Haonga

Mahakama ya Wilaya ya Mbozi, Songwe imemuachia huru mbunge wa Mbozi (Chadema), Pascal Haonga na wenzake wawili baada ya kukutwa hawana hatia katika kesi iliyokuwa ikiwakabili. Haonga na wenzake, Wilfredy Mwalusamba (katibu wake) na Mashaka Mwampashi wameachiwa huru leo mchana Ijumaa Agosti 10, 2018. Walikuwa wakikabiliwa na mashtaka matatu ya kufanya fujo na kuvuruga mkutano…

Read More

Uingereza yaipatia Tanzania Sh307 bilioni

Serikali ya Uingereza imetoa msaada wa Sh 307.5 bilioni kwa Tanzania ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono Rais John Magufuli katika elimu, mapambano dhidi ya rushwa na uboreshaji huduma za afya. Msaada huo umetangazwa leo Ijumaa Agosti 10, 2018 na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza, Penny Mordaunt alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais…

Read More

Askari wawili wahojiwa tukio la mwanahabari kupigwa

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema polisi waliokuwa zamu siku ambayo mwandishi wa habari wa Wapo Redio, Sillas Mbise alishambuliwa na askari, wameanza kuchunguzwa. Mbise anadaiwa kushambuliwa na polisi juzi Agosti 8, 2018 wakati wa mchezo kati ya Simba na Asante Kotoko ya Ghana uliofanyika katika Uwanja wa Taifa,…

Read More

Kalanga amalizana na CCM, aisubiri Chadema

Hatimaye maandamano ya wana-CCM wilayani Monduli kupinga Julius Kalanga kuwa mgombea pekee wa ubunge kupitia chama hicho yamegonga mwamba baada ya kada huyo kujitokeza peke yake kuchukua na kurejesha fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania nafasi hiyo. Kalanga aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema kabla ya kujiuzulu na kujiunga na CCM, iwapo atapitishwa…

Read More