Benki ilivyomwibia mteja kwa usanii

Baada ya Gazeti la JAMHURI kuchapisha habari ya kwanza kwenye toleo Na. 371 ikionyesha jinsi Benki ya BOA inavyoibia wateja nchini kwa maofisa wake kughushi nyaraka za wateja na kujipatia mikopo, sasa yameibuka mambo ya kutisha, JAMHURI linaripoti. Wamejitokeza wateja zaidi ya 50 wanaolalamika kuibiwa na maofisa wa BOA kwa nyakati tofauti, kwa utaratibu ule…

Read More

Barua ya wazi kwa Rais wa Tanzania

Je, GMOs ni Sera ya Serikali? Mheshimiwa Rais; Kwa heshima na taadhima, niruhusu mimi mtoto wa mkulima mdogo na mwananchi wa nchi yetu tukufu nikusalimu. Hali yangu mimi na wanafamilia wenzangu, ambao ni wakulima wadogo nchini, si njema kabisa. Mheshimiwa Rais, kama ujuavyo, sisi ni takribani asilimia zaidi ya 70 ya wananchi wote, na naamini…

Read More

Magufuli avunja rekodi

Rais John Magufuli katika kipindi chake cha uongozi cha miaka mitatu amefanya mengi ambayo hata wakosoaji wake wanakiri kuwa ni ya kupigiwa mfano. Kwenye toleo hili maalumu, tumeorodhesha baadhi ya mambo hayo yakilenga kuonyesha mafanikio makubwa katika kuimarisha nidhamu, uadilifu na uwajibikaji ndani ya utumishi wa umma na kukemea uzembe na kujenga ari ya kufanya…

Read More

Waenda Uingereza kuchangisha fedha za ‘mapambano’ Loliondo

Mgogoro wa masilahi katika Pori Tengefu la Loliondo (LGCA) unafukuta upya baada ya Watanzania takriban 20 kutarajiwa kusafiri kwenda nchini Uingereza wiki hii kuomba fedha za kuendeshea mapambano dhidi ya serikali. Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI umebaini kuwa harambee ya kukusanya fedha hizo imeandaliwa na asasi ya The Oakland Institute ya nchini Marekani. Fedha zinazotarajiwa kukusanywa,…

Read More

Mwenyekiti Baraza la Ardhi akataliwa

Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba Wilaya ya Moshi, James Silas, amekataliwa kuendelea kusikiliza shauri la ardhi namba 175/2017 lililopo mbele yake. Oktoba 6, mwaka huu, Donald Kimambo na David Kimambo waliandika barua wakimtaka Silas kujitoa kusikiliza shauri lao. Barua hiyo imeeleza kuwa wamechukua uamuzi huo baada ya Silas kufuta shauri lao bila kusikiliza…

Read More

Hongera Rais Magufuli

Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli imetimiza miaka mitatu tangu ilipoingia madarakani mwaka 2015. Rais Magufuli alishika uongozi nchi ikiwa inakabiliwa na matatizo mengi ya kiuchumi, kijamii na kimaadili. Hatuna kipimo sahihi cha kubainisha kazi zilizokwisha kufanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kwa miaka hii mitatu, lakini itoshe tu kusema…

Read More