Benki ilivyomwibia mteja kwa usanii
Baada ya Gazeti la JAMHURI kuchapisha habari ya kwanza kwenye toleo Na. 371 ikionyesha jinsi Benki ya BOA inavyoibia wateja nchini kwa maofisa wake kughushi nyaraka za wateja na kujipatia mikopo, sasa yameibuka mambo ya kutisha, JAMHURI linaripoti. Wamejitokeza wateja zaidi ya 50 wanaolalamika kuibiwa na maofisa wa BOA kwa nyakati tofauti, kwa utaratibu ule…