Usalama kazini tatizo Kiwanda cha Saruji Nyati
Mfanyakazi wa Kiwanda cha Saruji cha Nyati, Charles Reuben, amekufa akiwa kazini huku chanzo cha kifo kikidaiwa ni kufunikwa na kifusi cha makaa ya mawe. Reuben amekutwa na mauti hayo usiku wa kuamkia Julai 28, 2019 baada ya kuteleza na kutumbukia kwenye eneo linalopokea makaa hayo (coal mill) kwa ajili ya kuendesha mitambo ya kuzalisha…