Mshambuliaji mpya wa klabu ya Costal Union ya Tanga, Ali Kiba, ameanza kujinoa na wachezaji wa kikosi hicho huko Tanga tayari kwa msimu mpya wa ligi utakaoanza Agosti 22 2018.

Kiba ambaye pia ni Msanii wa Kimataifa kupitia Muziki wa kizazi kipya, ameanza kambi hiyo baada ya kujiunga na Coastal akisaini mkataba wa mwaka mmoja.
Nyota huyo amekuwa gumzo kubwa ndani ya jiji la Tanga na kwa mashabiki na wanachama wa Costal kutokana na usajili wa Kiba ambao haukutarajiwa na wengi.
Ikumbukwe Kiba amekuwa na umaarufu mkubwa zaidi katika tasnia ya muziki tofauti na mpira, japo ana kipaji kikubwa cha kusakata kambumbu.
Caostal wameanza kujifua tayari kwa maandalizi ya msimu mpya ambao utakuwa na idadi ya timu 20 kutoka 16 ilivyokuwa kwa 2017/18.

By Jamhuri