Mila za Wazanaki: Mwitongo na Muhunda
Baada ya makala ya juma lililopita juu ya lugha ya Kizanaki, naendeleza makala inayofafanua mila na tamaduni za kabila la Wazanaki. Eneo la Butiama linalojulikana kama “Mwitongo” linatokana na neno la Kizanaki lenye kumaanisha “mahame”, eneo ambalo lilikuwa na wakazi ambao walihamia sehemu nyingine. Kwa desturi chanzo kikuu kilichosababisha watu kuhama eneo moja kilikuwa kifo…