Kumbe ndio maana trafiki wanachukiwa
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikisikia na kuona jinsi wananchi wengi katika maeneo mbalimbali ya nchi hii, wanavyowalalamikia askari polisi wa kitengo cha usalama barabarani (trafiki). Siyo siri ndugu zetu hao wanachukiwa na wananchi wengi.