Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Agustine Ollomi
Juma Nyoso akiwa chini ya ulinzi wa Polisi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Agustine Ollomi, amesema hali ya majeruhi anaye fahamika kwa jina la Shabani Hussein, aliyedaiwa kupigwa hadi kuzirai na beki wa Klabu ya Kagera Sugar, Juma Nyoso, bado ni mbaya na yupo mikononi mwa madaktari huku mtumuhimiwa aliyetenda tukio hilo akishikiliwa na jeshi la polisi.

Nyosso anadaiwa kumpiga shabiki huyo muda mfupi baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera kati ya timu yake dhidi ya Simba uliomalizika kwa Simba kushinda mabao 2-0.

By Jamhuri