Biteko: Ushirikiano Tanzania,Canada katika sekta ya madini umeendelea kuimarika
Waziri wa Madini Dkt.Doto Biteko amesema ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Canada katika sekta ya Madini umeendelea kuimarika hususan katika masuala ya utafiti wa madini. Dkt.Biteko ameyabainisha hayo leo Junuari 19, 2023 mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Kyle Nunas Ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma. Dkt….