MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda amefunguka na kusema uwezo mkubwa wa Rais Magufuli na Demokrasia ya kweli ni jambo ambalo linawavutia wageni kuja Tanzania akiwepo Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame anayetarajiwa kuwasili nchini Jumapili.

Makonda amesema hayo leo akiwa katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam baada ya kuagana na Rais Magufuli ambaye ameelekea visiwani Zanzibar kushiriki sherehe za maadhimisho ya Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

“Amani Demokrasia ya kweli, upendo na uwezo wa mkubwa wa Rais Magufuli ndiyo msingi wa kuwavuta wageni kuja kutembelea hakuna mgeni ambaye anaweza kutembelea nchi ambayo haina upendo, amani na mshikamano. Tanzania chini ya uongozi wa Rais Magufuli inaendelea kuchanja mbuga katika nyanja za kidemokrasia hasa pia katika uwanja mwingine wa kidiplomasia na kuwafanya wageni waone sehemu nzuri ya kuja kutembelea,” alisema Makonda. 

Mbali na hilo Makonda amesema kuwa Rais Paul Kagame atawasili nchini Tanzania siku ya Jumapili ya tarehe 14 ambapo atakuwa nchini kwa ziara ya siku moja na kufanya mazungumzo na Rais John Pombe Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam.

By Jamhuri