Pigo kwa CHADEMA, Kampeni Meneja wa Godbless Lema Ajiunga na CCM

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Arusha kimepata pigo lingine baada ya Katibu Mwenezi wa CHADEMA ambaye pia alikuwa Meneja Kampeni wa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Gabrieli Kivuyo (kushoto) amekihama chama hicho na kujiunga na CCM.

Gabrieli Kivuyo amesema, amefikia uamuzi huo kutokana na utovu wa nidhamu uliopo ndani ya CHADEMA.

Hii ni muendelezo wa Wanachama na Viongozi wa CHADEMA kuendelea kukimbia chama hicho na kuhamia CCM kwa sababu mbalimbali, Viongozi wengi waliokiama na kuhamia CCM sababu ilikuwa ni kuridhishwa na utendaji kazi mzuri wa Serikari ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli, lakini huyu yeye amehama kwasababu yake kuwa Chama chao hakina nidhamu.