Ronaldo, Modric, Salah Vitani Mchezaji Bora, Messi, Mbappe Waenguliwa

Shirikisho la soka barani Ulaya limetangaza majina ya Nyota wanaoshindania tuzo ya Mchezaji Bora wa Ulaya UEFA kwa mwaka 2017/2018 ambao ni Cristiano Ronaldo wa Juventus, Luka Modric wa Real Madrid na Mohammed Salah wa Liverpool.

Hii ni baada ya kufanya mchujo wa wachezaji 10 kati ya hao ni washindi wa Kombe la Dunia mwaka huu.

Luka Modrić (Real Madrid na Croatia)
Mshindi wa Kombe la Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) 2018, Mchezaji Bora wa Dunia (Kombe la Dunia ‘FIFA World Cup’ 2018.

Cristiano Ronaldo (Real Madrid/Juventus and Portugal)
Mshindi wa Kombe la Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) mara tano na mfungaji Bora wa UEFA Champions League mwaka 2018, mshindi wa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia (Ballon d’Or) mara tano.

Mohamed Salah (Liverpool and Egypt)
Ana rekodi nyingi za michuano ya UEFA Champions League hasa katika msimu wake wa kwanza ndani ya Liverpool. Amefanikiwa kucheza fainali hizo na Hispania licha yakutolewa nje baada ya kuumia.

 

Wengine walioingia 10 Bora ni;

4 Antoine Griezmann (Atlético & France) – 72 points
5 Lionel Messi (Barcelona & Argentina) – 55 points
6 Kylian Mbappé (Paris & France) – 43 points
7 Kevin De Bruyne (Manchester City & Belgium) – 28 points
8 Raphaël Varane (Real Madrid & France) – 23 points
9 Eden Hazard (Chelsea & Belgium) – 15 points
10 Sergio Ramos (Real Madrid & Spain) – 12 points.

Tuzo nyingine ni;

Goalkeeper wa msimu: Alisson Becker, Gianluigi Buffon, Keylor Navas.
Beki wa msimu: Marcelo, Sergio Ramos, Raphaël Varane.
Kiungo wa msimu: Kevin De Bruyne, Toni Kroos, Luka Modrić.
Mshambuliaji wa msimu: Lionel Messi, Cristiano Ronaldo, Mohamed Salah.
Mchezaji wa kike wa Mwaka: Pernille Harder, Ada Hegerberg, Amandine Henry.
Mchezaji wa Ulaya wa Msimu: Diego Godín, Antoine Griezmann, Dimitri Payet.