TUNDU LISSU AWASILI NCHINI UBELGIJI KWA MATIBABU

Tundu lissu akipokelewa na wahuduma wa hospital alikofikia nchini Ubelgiji kwa matibau zaidi.
Tundu lissu aakisalimiana na wahuduma wa hospital na kupelekwa kwenye kitanda cha wagonjwa hospital hapo.
Tundu Lissu na Mkewe Kulia wakiwa kwenye chumba cha kulazwa wagonjwa hospital hapo.

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amewasili jijini Brussels, nchini Ubelgiji alikopelekwa kwa ajili ya matibabu zaidi na mazoezi ya viungo. Jana aliondoka katika Hospitali ya Nairobi alikolazwa kwa takribani miezi minne akipatiwa matibabu.