Walioficha mabilioni Uswisi wahojiwa
*Kwenye orodha wamo majenerali wa JWTZ
*Mboma, Sayore, Yona, Chenge, Mgonja ndani
*AG akiri kazi ni ngumu, aomba waongezwe muda
*Asema mwanga muhimu umeanza kuonekana
Kamati iliyoundwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuchunguza Watanzania walioficha fedha kwenye mabenki ughaibuni, imeshawahoji vigogo, wakiwamo mawaziri wa zamani, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, wanasiasa na wafanyabiashara maarufu.