M23 walia njaa

Waona giza nene mbele yao, Uganda yaonya vita inanukia
DRC yazidisha mashaka kwa Uganda, Watanzania waonya

Hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kukataa kusaini mkataba wa amani na kundi la waasi la M23, imepeleka kilio kwa kundi hilo, na sasa wanalia njaa uhamishoni nchini Uganda.

Read More

NUKUU ZA WIKI

Bill Getes: Kukumbuka ulipokosea ni muhimu

Ni vizuri  kusherehekea mafanikio lakini ni muhimu zaidi kukumbuka uliposhindwa awali.

Kauli hiyo ilitolewa na mfanyabiashara mkubwa  wa Marekani na Mwenyekiti wa Microsoft. Bill Gates.

Read More

Kwaheri Dk. Mvungi, turejeshe mabalozi wa nyumba 10

Wiki iliyopita ilikuwa ya majonzi makubwa kwangu, na naamini kwa Taifa letu kwa jumla.

Tumempoteza mwanasheria mahiri, Dk. Sengondo Edmund Mvungi, aliyevamiwa na majambazi nyumbani kwake Kibamba na kucharangwa mapanga. Baada ya Dk. Mvungi kucharangwa mapanga, alipelekwa Hospitali ya Mifupa Muhimbili (MOI) na baadaye akakimbizwa nchini Afrika Kusini, alikofia.

Read More

Al-Shabaab wapo Tanzania

Matukio ya ugaidi yanayoendelea sehemu mbalimbali hapa nchini, yanathibitisha pasi shaka kuwa kundi la al-Shabaab la nchini Somali tayari lina makazi yake hapa nchini Tanzania.

Oktoba 7, mjini Mtwara walikamatwa vijana 11 wakifanya mafunzo ya ugaidi katika Mlima wa Makolionga wilayani Nanyumbu, na walikutwa wanamiliki silaha za moto, mapanga na DVD 25 zenye miongozo ya mafunzo ya al-Shabaab. Hii ilithibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen.

Read More