WAZIRI MKUU AWAONYA VIONGOZI WAPYA WA SHIRECU
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wapya wa Chama Kikuu cha Ushirika Shinyanga wajipime kama wako tayari kuwatumikia wananchi na kama sivyo waachie ngazi. Ametoa onyo hilo jana (Ijumaa, Julai 13, 2018) wakati akizungumza na mamia ya wananchi wa kijiji cha Mwangongo na vijiji vya jirani mara baada ya kukagua soko la pamba kwenye…