WAZIRI WA KILIMO DKT.TIZEBA ATEMBELEA KIWANDA CHA MICRONIX-NEWALA

Waziri wa Kilimo Dr.Tizeba akiongea na Baadhi ya Wafanyakazi wa Kiwanda cha kubangua Korosho cha Micronix System ltd kilicho Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara ambacho Kimeajiri wafanyajazi 350.
Waziri wa Kilimo Dr.Tizeba akioneshwa aina za Korosho ambazo Tayari zimebanguliwa na kuwekwa kwenye vibakuli ili kupima Ubora Tayari kwa Kupakia Kushoto kwake ni mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo pamoja Meneja Uzalishaji wa ETG Ltd Sunir Mizar.
Waziri kilimo Dr.Charles Tizeba Akipanda Mche wa Mkorosho katika Kijiji cha Machombe,Kata Ya Marika kama Moja ya kuhamasisha upandaji wa Miche Mipya Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara.

Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba ametembea kiwanda cha kubangua Korosho cha Micronix System Limited kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara na kuzungumza na Viongozi wa kiwanda hicho juu ya kupandisha malipo kwa Vibarua wanaofanya kazi Kiwandani hapo.
Kwa Sasa mfanyakazi analipwa Kwati ya Shilingi elf7 mpaka elf8 kwa siku ambapo wanafanya kazi Kwa Siku 5 kwa Wiki.
Tayari uongozi kwa kiwanda hicho kwa  kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo wameahidi kulifanyia kazi Swala hilo.