Kairuki awataka machifu kuhimiza jamii kulinda miradi ya maendeleo
Na Mwandishi Wetu,JamhuriMedia,Same Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki amewataka machifu ambao ni viongozi wa kimila kuhamasisha jamii kulinda miundombinu ya miradi ya maendeleo. Waziri Kairuki ametoa wito huo wakati akisimika machifu wa Kipare kwenye hafla iliyofanyika kwenye Kata ya Suji wilayani Same mkoani Kilimanjaro. Amesema…
Waitara azindua ujenzi wa uwanja wa gofu wa kimataifa Serengeti
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Jenerali (Mstaafu) George Mwita Waitara ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa uwanja wa gofu ambao umebea jina la SERENGETI NATIONAL PARK GOLF COURSE wa kipekee duniani katika eneo la Fort Ikoma Wilayani Serengeti Mkoa wa Mara. Akizungumza katika hafla ya uwekaji…
KM 32 Wilyani Kyela kujengwa kwa lami
Serikali imesema itaendelea kutekeleza Sera yake ya kuunganisha mkoa kwa mkoa na wilaya kwa wilaya kwa barabara za lami ili kurahisisha usafiri na usafirishaji wa abiria, mazao na malighafi mbalimbali ili kukuza uchumi kwa haraka. Akizungumza wilayani Kyela wakati wa utiaji saini mkataba wa ujenzi wa barabara ya Ibanda hadi Kajunjumele (KM 22), Kajunjumele hadi…
Waliovamia eneo la hifadhi ya Nanyumbu wapangwa upya
Serikali imeamua kuwapanga upya wananchi wa vijiji viwili vya Mbagala Mbuyuni na Marumba wilayani Nanyumbu mkoani Mtwara ili kutatua migogoro ya matumizi ya ardhi na kuleta usalama kwenye maeneo hayo. Akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Wanika kata ya Mkonona tarafa ya Nanyumbu wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara tarehe 28 Desemba 2022 wakati wa ziara…
Ruvuma yakusanya mapato kwa asilimia 110
Mkoa wa Ruvuma umeweza kukusanya mapato kwa asilimia 110.8 katika mwaka 2021/2022. Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema katika kipindi hicho Halmashauri zote nane zimeweza kukusanya mapato ya zaidi ya shilingi bilioni 21 kati ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 19.33. “Nitumie fursa hii kuwapongeza wakurugenzi kwa kusimamia vizuri ukusanyaji mapato,nawakumbusha wakurugenzi…