JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kimataifa

Kiongozi wa upinzani wa Uganda Besigye afikishwa mahakamani

Mwanasiasa mkongwe wa Uganda Kizza Besigye na mshtakiwa mwenzake, Obeid Lutale wamefikishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Kampala, huku kukiwa na ulinzi mkali. Wawili hao wanakabiliwa na mashtaka manne yakiwemo ya kumiliki silaha kinyume cha sheria, tuhuma ambazo wanakanusha. Leo,…

WHO yachunguza mripuko wa ugonjwa usiojulikana DRC

Shirika la Afya Duniani WHO limesema hapo jana kuwa linaendelea na uchunguzi kuhusu mripuko wa ugonjwa usiojulikana uliogundulika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Katika mkoa wa Panzi, ulioko zaidi ya kilomita 700 kutoka mji mkuu Kinshasa, maambukizi 406 yameripotiwa…

Rais wa Korea Kusini Yoon atakiwa kujiuzuku kwenye chama chake

Rais Yoon Suk Yeol wa Korea Kusini ambaye alitangaza sheria ya kijeshi ametakiwa kuondoka kwenye chama chake cha People’s Power Party. Kiongozi wa chama hicho Han Dong-hoon aliwaambia waandishi wa habari “amemtaka rais huyo kujiuzulu” kutoka kwa chama. Hata hivyo…

Rais Korea Kusini atangaza hali ya hatari, jeshi lasimamisha shughuli za bunge

Rais wa Korea Kusini, Yoon Suk Yeol, ametangaza hali ya hatari muda mfupi uliopita, katika hotuba ya usiku wa manane. Amesema hatua hiyo ni muhimu ili kuilinda nchi kutokana na vikundi vya kikomunisti vya Korea Kaskazini na kuwaondoa watu wanaoipinga…

Uturuki: Kiini cha vurugu za Syria si ‘uingiliaji wa kigeni’

Uturuki yasema itakuwa kosa kujaribu kueleza kuwa matukio ya Syria yametokana na uingiliaji wa mataifa ya kigeni. Uturuki, ambayo inaunga mkono makundi ya waasi nchini Syria, imetupilia mbali wazo lolote la kwamba vurugu za kaskazini mwa Syria zimetokana na uingiliaji…

Israel yaishambulia Lebanon huku Hezbollah ikilenga kituo cha kijeshi

Israel imesema ililenga shabaha nchini Lebanon Jumatatu jioni baada ya kuapa kulipiza kisasi kwa shambulio la Hezbollah kwenye kituo cha kijeshi, huku pande zote mbili zikilaumiana kwa kukiuka usitishaji vita wa wiki iliyopita. Takriban watu tisa waliuawa na mashambulizi ya…