JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

NUKUU ZA WIKI

Mwalimu Nyerere: Tuendeleze 
demokrasia tupate maendeleo

“Jambo kubwa kwa maendeleo ya nchi yetu ni kuendeleza demokrasia yenyewe na siyo muundo unaoiendesha. Jambo hili litakapoletwa ili liamuliwe na mkutano wa Chama, hoja zitakazoongoza uamuzi huo lazima ziwe na uhusiano na hali halisi na mahitaji ya Tanzania ya wakati huo.”

Haya ni maneno ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

KELVIN CHRISTOPHER ‘KIBA GITA’:

 

Prodyuza anayetamani  kumiliki kituo cha redio

Imekuwa jambo la kawaida kwa vijana wengi kukaa vijiweni, kwa kisingizio kuwa Serikali imeshindwa kuwapatia ajira.

FC Lupopo yasifu wachezaji wa Tanzania

*Huenda Kaseja akasajiliwa huko

Katika hali inayoonesha kuwa wanandiga wa Kitanzania wanaosakata kabumbu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wanakubalika, Klabu ya Soka ya FC Lupopo imesema wachezaji kutoka Tanzania wanapendwa nchini humo kutokana na uwezo wao kisoka.

Tenisi wajihami Afrika Mashariki, Kati

Timu ya Taifa ya Tenisi inayoshiriki mashindano ya Afrika Mashariki na Kati kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15, imeondoka leo kwenda Nairobi, Kenya kushiriki mashindano ikiwa na matumaini ya kushinda.

Kodi ya simu inarejesha ‘Kodi ya Kichwa’

Taifa letu lipo katika mtikisiko mkubwa. Kuna mjadala mkubwa unaoendelea juu ya uanzishwaji wa kodi ya kumiliki simu. Kodi hii inatajwa na wengi kuwa ni kama kodi ya ‘Kichwa’ iliyobatizwa jina la kodi ya maendeleo baada ya Uhuru.

Tanzania imefikia kilele katika dawa za kulevya

Dawa za kulevya zinazidi kuchafua jina la Tanzania. Zimekuwapo taarifa za orodha ya watu wanaotumia au kuuza dawa hizo hapa nchini, lakini kadri siku zinavyopita tatizo linazidi kuwa kubwa kwa kiwango cha kutisha. Katika hali isiyo ya kawaida, Mtanzania aliyeko kifungoni nchini China ameamua kuanika ukweli wa kinachoendelea Tanzania.