Category: MCHANGANYIKO
Ukabila dhidi ya Profesa Maji Marefu ni upuuzi
Wiki iliyopita, Mkuu wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, Mrisho Gambo, alishuhudia namna Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani (Profesa Maji Marefu), anavyopigwa vita ya kikabila na baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali jimboni humo.
Kimwili CCM, rohoni ni Upinzani
Nimemsikia Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, akisema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hakina hazina ya viongozi kama iliyonayo Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Tuwape moyo viongozi wachapakazi
Mhariri,
Wakati umefika kwa Watanzania kuzungumza na kupongeza viongozi wachapakazi wachache tulionao nchini. Hii tabia itafanya viongozi wengine wengi wawaige viongozi wachapakazi.
Nasema hivi kwa sababu mara nyingi Watanzania wamekuwa na tabia ya kulaumu bila kuchambua viongozi wale wanaofanya kazi kwa uadilifu. Siandikii mate ilhali wino upo.
Wachezaji wa kigeni wanazididimiza Tanzania, England soka la kimataifa
Tangu ilipofuzu kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zilizofanyika nchini Nigeria mwaka 1980, ikatolewa mapema ikiwa kundi moja na wenyeji, Misri na Ivory Coast, timu ya soka ya taifa ya Tanzania hadi sasa haijaweza kuifikia tena hatua hiyo na hakuna matumaini yoyote kama itafanya hivyo tena.
CWT: Mkombozi au mnyonya walimu?
*Nusu ya mapato yake yanatumika makao makuu
*Walimu wanaendelea kukamuliwa asilimia mbili
Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa, katika Mkutano wa Bunge uliomalizika hivi karibuni alichangia Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kuhoji matumizi ya mabilioni ya shilingi yanayofanywa Makao Makuu ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT). Ifuatayo ni sehemu ya hotuba ya mbunge huyo.
Tumechagua kujenga taifa la wajinga
Kwa muda sasa nimekuwa nikifuatilia mwenendo wa elimu nchini. Nafuatilia kilio na matangazo yanayotolewa kila pahala, yakielezea wanafunzi zaidi ya 5,000 wanaomaliza elimu ya msingi na kufaulu mtihani wa darasa la saba huku hawajui kusoma na kuandika. Si hilo tu lakini nafuatilia pia kaulimbiu kuwa ‘Ualimu ni wito’.