JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Tuache kufyatua maneno

Habari yenye kichwa cha maneno, “Waziri achafua hewa mazishi ya Padri Z’bar” iliyochapishwa Februari 21, 2013, ilinikumbusha agizo la Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa (pichani chini), aliyetuasa akisema “Kama hujafanya utafiti, huna haki ya kuzungumza”.

NUKUU ZA WIKI

Nyerere: Tushirikishe watu katika maendeleo

“Kama maendeleo ya kweli ni kuchukua mahali, watu wanapaswa kushirikishwa.”

Hii ni sehemu ya maneno ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere katika kitabu chake cha Uhuru na Maendeleo, 1973.

Tunataka Katiba halisi  ya kudumu

Kama tujuavyo, hivi sasa Taifa letu liko katika mchakato wa kutafuta Katiba mpya ya nchi.

Katiba tunayotafuta sasa itakuwa nafasi ya katiba ya kudumu iliyoanza  kutumika mwaka 1977. Katiba ya nchi tunayotaka kuachana nayo imedumu kwa mbinde kwa sababu ina kasoro nyingi zilizoanza kupigiwa kelele tangu mwaka 1992, wakati Tanzania ilipoingia kwenye mfumo wa vyama vingi.

‘Privatus Karugendo anapotosha’

Privatus Karugendo, katika makala yake iliyochapishwa chini ya kichwa cha maneno, “Papa Benedict wa XVI Mfungwa wa imani anayetaka kuwa huru”, iliyoandikwa Februari 17, 2013, kurasa 11, 12 na 13, angeweka wazi kwamba Papa Benedict huyo aliwahi, kabla ya Aprili 5, 2009, kumvua madaraka ya shughuli za upadri, pengine nisingekuwa na hamu ya kuandika makala haya.

Udini sasa nongwa (1)

 

Siku za karibuni kuanzia wakati ule wa Sensa ya Watu na Makazi, neno UDINI limekua na linasikika mara kwa mara. Katika baadhi ya magazeti kama JAMHURI, kuna mfululizo wa makala za udini, mathalani makala za Ndugu Angalieni Mpendu – FASIHI FASAHA.

CCM irudishe mali za umma serikalini

Tanzania ilikuwa nchi inayofuata mfumo wa chama kimoja hadi mwaka 1992, wakati nchi wahisani za magharibi ziliposhinikiza nchi zote duniani zinazoendelea, kuanzisha mfumo wa vyama vingi kama ishara ya kujenga misingi bora ya demokrasia kwa jamii.