Latest Posts
MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE
Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (9)
Katika sehemu ya nane, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alisema Rais ndiye aliyekiri kosa la Zanzibar kuingia katika OIC na pili ndiye aliyelazimika kukiri kule Dodoma kwamba utaratibu wa kushughulikia hoja ya Utanganyika ulikosewa lakini mawaziri wake mara zote mbili walitulia tu nakumuacha Rais ndiye akiri kosa na kubeba lawama. Ifuatayo ni sehemu ya kitabu cha Mwalimu Nyerere alichokiandika mwaka 1994 cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Endelea…
Katiba ya nchi yetu, na utaratibu tunaojaribu kujenga, vinataka kuwa katika hali kama hiyo, Mawaziri ndiyo wawajibike, na hivyo kumlinda Rais, si Rais awajibike, na kuwalinda Mawaziri wake, na tena kwa kosa ambalo si lake. Watu walioshindwa uongozi Bungeni, hata tukafikishwa hapa tulipo leo, ni Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa CCM.
Uhuru ulio wa kweli ni uhuru wa kiuchumi
Watanzania jana waliadhimisha miaka 52 ya Uhuru wa Tanganyika (Tanzania Bara). Maadhimisho haya yamekuja huku Afrika na dunia ikiwa katika simanzi kubwa kutokana na kifo cha Mzee Nelson Mandela (95), Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini.
KAULI ZA WASOMAJI
JAMHURI linatufaa kuhusu JWTZ Hakika ni ukweli usiopingika kuwa habari zinazochapishwa kwenye Gazeti Jamhuri kuhusu vikosi vya askari wetu wa JWTZ wanaolinda amani nchini Congo zimekonga mioyo yetu na zimetuongezea shauku ya kulipenda jeshi letu, hasa sisi tuliopo mpakani…
Nazuiwa kumwona Jaji Mkuu Tanzania
Mhariri,
Nimekuwa nikifuatilia haki yangu katika mahakama kwa miaka 14 sasa bila mafanikio. Kwamba nimekuwa nikifanya jitihada za kuomba kukutana na Mheshimiwa Jaji Mkuu, lakini hadi sasa sijafanikiwa kutokana na kunyimwa nafasi hiyo na watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Serikali itutatulie uhaba wa maji Komuge, Rorya
Mhariri,
Ninaona fahari kutumia nafasi hii katika Gazeti Jamhuri kuifikishia Serikali kilio cha wananchi katika kata ya Komuge, Wilaya ya Rorya mkoani Mara, ambao kwa muda mrefu sasa wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji.
FASIHI FASAHA
Lissu ni malaika, waziri au mwanasiasa?
Ni takriban wiki tatu sasa tangu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kipate mtikisiko mkubwa, mithili ya pata shika na nguo kuchanika, baada ya Kamati Kuu (CC) ya chama hicho kuwavua nyadhifa zote viongozi wake watatu.