JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Pinda agongana na bilionea Dar

*Ni Ally Awadh wa kampuni ya mafuta ya Lake Oil
*Atuhumiwa kumfanyia unyama mtumishi wake
*Polisi Oysterbay, Kanda Maalumu wamgwaya

[caption id="attachment_1591" align="alignleft"]Mlalamikaji anayedaiwa kupigwa na mabaunsa wa mfanyabiashara bilionea Ally Awadh (Lake Oil)[/caption]Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ameamua “kujipima uzito” dhidi ya bilionea Mtanzania, Ally Edha Awadh ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Lake Oil ya Mikocheni jijini Dar es Salaam inayoagiza, kuuza na kusafirisha mafuta na biashara nyingine nyingi.

Awadh anayetajwa kama mmoja wa mabilionea vijana nchini, amefunguliwa mashitaka Polisi ya kumteka, kumdhalilisha kinyume cha maumbile na kumpora mali mmoja wa wafanyakazi wake.

Uamuzi wa Waziri Mkuu Pinda umekuja baada ya Jeshi la Polisi nchini, katika kile kinachoonekana ni kumgwaya bilionea huyo, kupuuza kumsaidia mlalamikaji huyo mwenye umri wa miaka 32. Kwa sababu za kiutu na za kitaaluma, jina la mlalamikaji tunalihifadhi kwa sasa.

Kitanzi cha JK

Wizara ya Maliasili yatajwa kuwa mtego kwa Kikwete

Pinda, Mwamunyange, Mwema watakiwa kupima uzito

Rais Jakaya Kikwete, akiwa anatarajiwa kulisuka upya Baraza la Mawaziri, kuna kila dalili kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa sasa ndio imebaki kuwa kitanzi kinachotishia uhai wa Serikali yake.

MKATA MITAA

WAWATA St. Joseph na bei za vyakula za ‘kitalii’

Kwa kawaida watu wanyonge wamezitambua nyumba za ibada kama sehemu ya ukombozi! Haishangazi kuwaona kina mama, kina baba, watoto, wazee na watu wasiojiweza wakikimbilia makanisani na misikitini kunapotokea vurugu.

FASIHI FASAHA

Mandela  ataenziwa au atakumbukwa?

Ni muda wa wiki tatu sasa, dunia imepata mzizimo na simanzi kutokana na kifo cha mtoto wa Afrika, shujaa, mpenda haki na usawa na kipenzi cha dunia, mtoto huyo ni Nelson Mandela. “Madiba.”

Mawaziri wameondoka, Kikwete rekebisha sheria

Mawaziri wameondoka, Kikwete rekebisha sheria

 

Wiki iliyopita kwa mara nyingine nchi yetu imepata mtikisiko. Imepata mtikisiko kutokana na mawaziri wanne kupoteza nyadhifa zao. Haya yametokea Ijumaa ya Desemba 20, 2013. Mawaziri hawa; Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa), Mathayo David Mathayo (Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi) na Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani), wameacha sura mbili.

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

 

Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (11)

 

Katika sehemu ya kumi, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alisema kwa hiyo Waziri Mkuu alipomwambia Rais kwamba hoja ya Serikali Tatu ikijadiliwa Bungeni yeye mwenyewe atakuwa na utatizi wa uamuzi, alikuwa anajisemea kweli yake. Alikuwa katika hali hii ya “dilemma”. Baadaye, kama tunavyojua, alipoambiwa kuwa asipokubaliana na wenzake ataachwa katika mataa, aliamua kusarenda na wote wakaunga mkono hoja ya Utanganyika.

Ifuatayo ni sehemu ya kitabu cha Mwalimu Nyerere alichokiandika mwaka 1994 cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Endelea…

 

Hawa si watu wajinga, na wala  si wapumbavu; wanajua wafanyalo. Wamefanya uamuzi huu wakijua matokeo yake. Kwa hawa sasa, makosa ya “Wazanzibari” yawe ya kuvunja Katiba au ya aina nyingine, kwao sasa ni faraja; ni hoja ya kudai Utanganyika. Hawa hawawezi tena kutaka makosa hayo yazungumzwe na yasahihishwe; maana yakisahihishwa kama lilivyosahihishwa lile la OIC msingi wake wa hoja yao utabomoka.