Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP) ambaye pia ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Abdul Nondo, amezungumza kwa mara ya kwanza na waandishi wa habari baada ya kuachiwa huru katika mahakama ya Iringa hapo jana.

Katika Mazungumzo yake Nondo, amewashukuru watanzania kwa kupaza sauti zao, jeshi la magereza mkoani Iringa, Mawakili wake, pamoja na mtandao wa wanafunzi na taasisi ya haki za binadamu.

By Jamhuri