Baada ya kuidhinishwa na Baraza la Serikali ya China, kamati ya Ushuru wa Forodha ya China imeamua kuwa itasimamisha upunguzaji wa ushuru wa Forodha kwa bidhaa 128 za aina 8 zinazoagizwa kutoka Marekani kuanzia jana tarehe 2 Aprili, huku ikiongeza ushuru wa Forodha kwa bidhaa hizo.

Ikumbukwe kuwa tarehe 22 Machi, Rais Donald Trump wa Marekani amesaini kumbukumbu ya kuiwekea China vikwazo kwa mujibu wa matokeo ya ripoti kuhusu ukaguzi wa kipengele cha 301 cha sheria ya biashara, na kuagiza kutoza ushuru mkubwa Wa Forodha kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka China, na kuweka Kikomo kwa kampuni za China kuwekeza na kununua kampuni za Marekani.

Hili limefanyika Marekani kuwawekea vikwazo China je kwa Tanzania hatuwezi na sisi tukatumia mfumo huo ili kuiongezea Thamani bidhaa zetu za ndani kwa kuwawekea ushuru Mataifa yanayoingiza bidhaa zao nchini kwa wingi kama China ili bidhaa zetu zikanunulika kwa bei ya chini na tukaachana na za nje?

By Jamhuri