Mkuu wa Jeshi la Polisi, Simon Siro amefanya mabadiliko ya Makamanda katika baadhi ya mikoa kama ifuatavyo.
1. SACP Deusdedit Nsimeki aliyekuwa Makao Makuu ya Upelelezi anakwenda kuwa RPC Simiyu.

2. SACP Ulrich Matei aliyekuwa RPC Morogoro, anakwenda kuwa RPC Mbeya.

3. Kaimu RPC Mkoa wa Mbeya, ACP Mussa Taibu amehamishiwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi

4. SACP Wilbroad Mutafungwa aliyekuwa RPC Tabora, anakwenda kuwa RPC mkoa wa Morogoro

5. ACP Emmanuel Nley toka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi anakwenda kuwa RPC Tabora

6. ACP Stanley Kulyamo aliyekuwa Ofisa Mnadhimu Mkoa wa Geita anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha TAZARA.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa, imesema mabadiliko hayo yanalenga kuongeza juhudi za kuzuia ajali zilizotokea mara kwa mara katika baadhi ya Mikoa.

By Jamhuri