Pongezi wana JAMHURI

Nawapongeza wafanyakazi wa Gazeti Jamhuri kwa kuanika wazi majina ya wauza unga katika toleo lililopita. Lakini kwanini serikali yetu isiwatie kitanzini kama huko China? Pia si hao tu, mafisadi nao watunguliwe risasi wazi wazi iwe fundisho kwa wengine wenye nia ya kufanya uovu huo.

 

Justus Julius Mwombeki, Bukoba

0753 191 029

Tuchangie maendeleo ya nchi

Hivi ni nani anawajibika kuchangia maendeleo ya nchi yetu Tanzania? Maana kila jambo likipitishwa linapingwa. Baadhi ya wanahabari badala ya kuhamasisha wananchi kuchangia maendeleo ya nchi yao wao kazi yao ni kuwakatisha tamaa. Hivi tunatoa fundisho gani kwa watoto wetu?

 

Mpenzi wa Jamhuri

0755 870 957

 

Wanahabari msiijibie serikali

Ni vema serikali ikajibu hoja za Jumuiya na Taasisi za Kiislam, badala ya ninyi [wanahabari] kuwa wasemaji wa serikali. Bila hivyo, tambueni kuwa kuandika/kujibu kwenu hakumalizi/hakufuti msamiati huo wa mfumo Kristo kwa sura moja tu ya kila anayesemwa dini yake kuwa na jicho la chongo.

 

Msomaji wa JAMHURI

0715 478 322

 

Unyama utaisha lini Tanzania?

Unyama utaisha lini. Huyo mfanyabiashara Mesenja Mayanda anaziamini sana pesa zake au kaiweka serikali mfukoni mwake ndiyo maana anajichukulia sheria mkononi?. Pole mzee Damas Masasila kwa kubomolewa nyumba zako na kuachwa bila makazi wewe na familia yako ya mke na watoto huko Geita.

 

Emmanuel Tungu Mashala, Igunga

0757 289 362

 

Mipango mingi isiyotekelezeka

Tanzania imejaliwa kuwa na watendaji wenye mipango lukuki isiyotekelezeka, hata inayotekelezwa siyo kwa asilimia zote, mfano tumeambiwa wauza unga ni vigogo walioko hata serikalini na wengine wametajwa kwa majina, lakini mbona katika hao waliotajwa na hili gazeti hatuwaoni hao viongozi?

 

Heze, Mwanza

0769 316 154

 

Serikali idhibiti dawa feki

Kwanini nchi yetu ya Tanzania yenye Serikali, Mamlaka ya Dawa na Chakula (TFDA), Polisi, Jeshi mipakani, mbwa na farasi wanaotengewa bajeti ya mamilioni ya fedha kila mwaka, lakini unaambiwa kuna DICLOFENIC feki mitaani? Dhamana ya maisha yetu iko kwa nani?

 

Mkereketwa wa Tanzania

0784 504 089

 

Serikali iisaidie familiya hii

Ndugu Mhariri, pole kwa kazi. Nimesoma habari ya unyama unaodaiwa kufanywa na mfanyabiashara Mesenja Mayanda na ofisa mtendaji kwa kubomoa makazi ya mzee Damas Masasila na familia yake wilayani Geita. Kwanini serikali inaacha wananchi wanyonge wanateswa kiasi hicho?

 

Raia mwema

0754 960 096

 

By Jamhuri