JAMHURI linatufaa kuhusu JWTZ

 

Hakika ni ukweli usiopingika kuwa habari zinazochapishwa kwenye Gazeti Jamhuri kuhusu vikosi vya askari wetu wa JWTZ wanaolinda amani nchini Congo zimekonga mioyo yetu na zimetuongezea shauku ya kulipenda jeshi letu, hasa sisi tuliopo mpakani na Congo. Endeleeni kukaza buti katika kutujuza habari na makala motomoto, tuko pamoja.

 

Kamazima Kyaruzi, Kigoma

0752 333 487

 

Namuunga mkono Magufuli

 

Ninampongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli, kutokana na utendaji kazi wake mzuri unaozingatia maslahi ya taifa. Ninampongeza sana kiongozi huyo kutokana na msimamo wake imara katika Wizara ya Ujenzi. Mwenyezi Mungu azidi kumbariki siku zote.

 

Bernard Kilala, Geita

0755 818 975


Mungu wabariki wana JAMHURI

 

Ninawapongeza waandishi wa Gazeti Jamhuri kutokana na ushirikiano mlioonesha katika kuandaa gazeti hili kwani siyo kazi ndogo, Mungu awabariki. Endeleeni kufanya kazi kwa juhudi, maarifa na ushirikiano bila kutegeana wala kutofautiana kimaslahi. Gazeti hili liko kwenye soko, tena najua ninyi ni wasomi makini, msiangushe taifa na sisi wasomaji wenu.

 

C.M. Nyakwar Otwalo, Shirati – Rorya

0784 668 841

 

Serikali iboreshe makazi Dar

 

Nadhani Serikali iboreshe makazi ya watu katika maeneo ya Kinondoni, Tandale, Manzese, Mikocheni, Vingunguti, n.k. kwa kutenga eneo la Mabwepande kwa ajili ya kujenga makazi ya kisasa na kuwahamishia huko wakazi wa maeneo niliyoyataja hapo juu kupisha ujenzi wa makazi ya kisasa kwa ajili ya kuwapangisha wananchi ili kujiongezea kipato na kupunguza tatizo la ukosefu wa makazi bora jijini Dar es Salaam.

 

Daniel, Kinondoni – Dar es Salaam

0658 313154


Zitto, Dk. Kitila wameonewa

 

Napenda kutoa ushauri kuhusu kutofautiana kwa viongozi wa CHADEMA. Ukisoma utete wa Kabwe Zitto na Dk. Kitila kuhusu waraka wa kufanya mabadiliko ya uongozi ndani ya chama, hiyo siyo uhaini wala kukisaliti chama, mimi nawaunga mkono. Ninamshangaa mwanasheria wa wa chama hicho Tundu Lissu, kwani hajaonesha uweledi katika hili bali ameonesha ushabiki wa upande mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu. Hajatenda haki. Marando Mabere hebu okoa CHADEMA.

 

C.M. Nyakwar Otwalo, Shirati – Rorya

0784 668 841

 

Lowassa okoa elimu Tanzania

 

Ni dhahiri kwamba katika Uchaguzi Mkuu ujao (mwaka 2015), Waziri mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, ndiye chaguo la Mungu, ingawa alidharauliwa, alitukanwa na kutemewa mate. Kwa kweli aliumia sana, ila ninamwomba atakapoingia katika ufalme wake asilipize kisasi, bali awasamehe bure watu wote walioshiriki kumwonea na kumuudhi, na zaidi awe hodari na mwenye moyo wa ushujaa.

 

Msomaji wa JAMHURI

0788 363 891


Serikali iache uonevu huu

 

Kwanini Serikali inashindwa kuweka mipaka katika maeneo ya wazi ili wananchi wasiyamavie na kujenga makazi. Ajabu ni kwamba Serikali hushtuka baada ya miaka mingi tangu watu walipovamia na kujenga makazi, hivyo kuwabomolea! Je, huo ndio utawala bora? Wakazi wa kijiji cha Kabange mkoani Katavi wamekubwa na tatizo hilo. Huo ni unyanyasaji unaotokana na uzembe wa Serikali.

 

Malimi Ng’halanga, Tumaini – Katavi

0782 356 435

 

Lowassa ukoe elimu Tanzania

 

Wakati Mheshimiwa Edward Lowassa akiwa Waziri Mkuu wa Tanzania, alisimamia vizuri mpango wa elimu ikiwa ni pamoja na kusimamia ujenzi wa shule za sekondari katika kila kata hapa nchini. Ni dhahiri tungekuwa tumepiga hatua kubwa sana katika elimu kuliko ilivyo sasa, ambapo elimu inadinimia! Mheshimiwa ninakuomba Lowassa okoa elimu Tanzania. Mungu akubariki.

 

Msomaji wa JAMHURI

0788 363 891

By Jamhuri