Uongozi wa Klabu umeuvunja rasmi mkataba na kocha wake msaidizi Irambona Masoud Djuma kuanzia leo Oktoba 8, 2018
Taarifa rasmi iliyotolewa na klabu hiyo imesema uamuzi huo umekuja baada ya mazungumzo kwa pande zote mbili hivyo ni kwa faida ya klabu na kwa maslahi ya pande zote
Aidha, Djuma amesema kuwa hakutegemea kama siku moja angefika Simba SC, anashukuru sana Wanachama na Mashabiki wa Simba na kuongeza kuwa kila lenye mwanzo lina mwisho

By Jamhuri