Uongozi wa Simba umesema leo ndiyo siku ya mwisho kwa wanachama wa timu hiyo kuchukua fomu kwa ajili uya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa klabu, Haji Manara, amewasihi wanachama wa klbu kujitokeza leo Jumatatu ili kuhakikisha wanapata haki yao kikatiba.

Aidha Manara amewataka wanachama kuitumia Jumatatu ya leo vizuri kwa ajili ya kuchua fomu hizo maana hakuna uwezekano wa siku kuongezwa.

Simba inatoa msisitizo huo ili kuja kupata rasmi viongozi watakaoiwezesha kuja kuanza kazi ikiwa katika muundo mpya wa kimabadiliko.

Klabu hiyo itafanya uchaguzi wake mkuu Novemba 3 2018 kwa ajili ya kuwapata viongozi wake wapya baada ya utawala uliopo madarakanani kumaliza muda wake.

By Jamhuri