Maandamano yazuka Kampala kupinga kukamatwa mbunge Bobi Wine

Kikosi cha Usalama kikizima Moto uliwashwa na Waandamanaji
… wakiwa kwenye ulinzi mkali dhidi ya waandamanaji

Vikosi vya usalama nchini Uganda wamewakamata watu 10 waliojihusisha na maandamano ya kupinga kukamatwa kwa Mbunge wa upinzani, Bobi Wine ambaye alikamatwa na kushitakiwa kwenye Mahakama ya Kijeshi wiki iliyopita. Shughuli za Biashara zimesimama katika Jiji la Kampala, leo Mchana kutokana na makabiliano makubwa kati ya Vikosi vya usalama dhidi ya Wananchi ambao waliojitokeza kwenye maandamano hayo.

Wandamanaji wamechoma moto magurudumu ya magari, wamerusha mawe pamoja na kuweka vizuizi Barabarani.