Mwanza Madereva wa Daladala wanaofanya safari zao Airpot Nyashishi na Kisesa Nyashishi wilayani Misungwi wamelazimika kugoma baada ya Sumatra kuongeza ruti bila kuongeza nauli.
Madereva hao wamelalamikia kitendo hicho kwakuwa ruti iliyopangwa sumatra haijatoa bei elekezi nauli itakuwa sh
Ngapi, kutokana na umbali.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza Anthon Bahebe ameliomba Jeshi la Polisi kitengo cha Usalama barabarani pamoja na mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa Majini na nchi kavu sumatra kusimamia suala hilo ili kuepusha adha wanayoipata Abiria.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha Madereva wa Daladala mkoani Mwanza Hassan Dede amekiri kuwepo kwa suala hilo na kusema kuwa bado kuna baadhi changamoto katika ruti hiyo hali ambayo imekuwa ikisababisha kuwepo kwa tatizo hilo.
Akizungumzia changamoto hiyo afisa leseni wa sumatra mkoani Mwanza Daniel Chilongani amesema kuwa tayari mamlaka hayo yanaendelea kushughulikiwa.

By Jamhuri