Billie Jean King akosoa mfumo wa seti tano

Mfalme wa zamani wa mchezo wa Tenisi mwanamke Billie Jean King amependekeza kuwa mfumo wa kucheza seti tano kwa wanaume michuano ya Gland slam usitumike katika mchezo wa mwisho.

Mchezaji huyo wa zamani ambaye alishinda mataji 12 ya Gland yakiwemo sita ya Wimbledon, amesema mfumo huo kwa upande wa wanaume umekuwa ukichukua muda mwingi kucheza , amependekeza kuwa mfumo huo utumike kwa wanawake .

Amesema mechezo unaochukua muda mwingi na ratiba iliyojaa michezo mingi ni sababu iliyosababisha majeraha makubwa kwa nyota za mchezo huo Andy Murray, Rafael Nadal, Djokovic na Stan Warinka katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.

By Jamhuri