Klabu ya Simba imeendelea kuweka rekodi kwa msimu wa pili mfululizo kuwa ni timu ya kwanza kwa kutoa mchezaji bora wa mwezi wa Ligi Kuu Bara.

Msimu huu mshambuliaji Mnyarwanda mwenye asili ya Uganda Meddie Kagere ndiye alikuwa mchezaji bora wa mwezi Agosti msimu huu baada ya kucheza michezo mwili.

Msimu wa uliopita Simba ndiyo ilifungulia kwa kutoa mchezaji bora wa mwezi ambaye alikuwa ni Mganda Emmanuel Okwi alikuwa mchezaji bora wa mwezi Agosti 2017 huku akiweka na rekodi ya kuweka ya ‘hat trick’ ya kwanza ligi kuu.

Hata hivyo msimu wa mwaka 2016/17 mchezaji bora wa mwezi wa kwanza alikuwa ni John Bocco ambaye alikuwa Azam FC na sasa anakipiga katika klabu ya Simba na msimu uliopita alikuwa mchezaji bora wa mwezi Januari.

By Jamhuri