Mkuu wa mkoa Geita ,mhandisi Robert Luhumbi kushoto akiwa na Mtakwimu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Douglas Masanja akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utafiti wa mapato na matumizi ya Kaya binafisi Tanzania Bara wa mwaka 2017/18. 
Katibu tawala wa Mkoa wa Geita,Celestine Gesimba akimkaribisha mkuu wa mkoa kuzungumza na waandishi wa habari juu ya utafiti wa mapato na matumizi ya kaya binafsi. 
Mtakwimu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Douglas Masanja  akiteta jambo na mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari Mkoani humo. 
 
 
Wananchi Mkoa wa Geita wametakiwa kutoa ushirikiano kwenye zoezi la utafiti wa mapato na matumizi kwenye Kaya binafsi ili kutoa takwimu za hali ya umasikini zitakazosaidia serikali na wadau wengine kutathimini hatua zilizofikiwa katika kutimiza malengo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
Miongoni mwa Malengo hayo ni pamoja na yale yaliyoainishwa katika mpango wa pili wa maendeleo ya miaka mitano pamoja na maendeleo endelevu.
Kata, Vijiji, Mitaa na vitongoji 34 mkoani humo vinatarajia kufanyiwa utafiti huo ili kupata taarifa zinazohusu Kaya na wanakaya, Uzazi na unyonyeshaji, elimu, afya, uraia, uhamiaji, ulemavu, bima, hali ya ajira, biashara na mapato ya kaya na makazi ya kaya.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi alisema utafiti huo utasaidia kuweka misingi katika kutambua viashiria vya kiuchumi, ajira na ustawi wa jamii vitakavyofuatiliwa kwa kipindi husika na kupata makadirio ya jumla ya mwenendo wa matumzi ya kaya ili kuandaa fahirisi za bei.
“Napende kuwahakkisa wananchi wa mkoa wetu kuwa katika kutekeleza maagizo ya serikali ,uongozi wa mkoa umeendelea kuhimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kutimiza azma ya serikali ya awamu ya tano ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda na yenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025”Alisema Luhumbi.
Amendelea kusema madhumuni ya utafiti huu wa mapato na matumizi ya kaya binafsi Tanzania Bara wa mwaka 2017/18 ni kutoa takwimu za hali ya umasikini na takwimu nyingine ili kusaidia serikali na wadau wengine kutathmini hatua zilizofikiwa katika kutimiza malengo mbali mbali ya kitaifa na kimataifa yakiwemo yale yaliyoanishwa katika mpango wa pili wa Taifa wa maendeleo wa miaka mitano (2016/17-2020/21) na malengo wa maendeleo endelevu.
Mtakwimu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Douglas Masanja alisema azma ya serikali ni taifa kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 hivyo kutokana na misingi hiyo zinatakiwa ziwepo taarirfa sahihi kutoka kwa wananchi.
Zoezi la utafiti ambalo linafanyika nchi nzima limeanza Desemba Mosi mwaka jana na linatarajiwa kukamilika mwezi Novemba mwaka huu.

By Jamhuri