Mgombe wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. ๐—ฆ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ฎ ๐—ฆ๐˜‚๐—น๐˜‚๐—ต๐˜‚ ๐—›๐—ฎ๐˜€๐˜€๐—ฎ๐—ป amesema CCM imeendelea kumuenzi Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere katika misingi ya utawala bora.

Dkt. Samia amesema katika kumuenzi Hayati Mwl. Nyerere hatuwezi kumtenganisha na misingi ya kiitikadi na kifalsafa aliyoijengea nchi yetu ambayo ilibebwa na dhana kama vile uhuru na umoja, kujitegemea, kazi pamoja na wajibu na dhana zingine muhimu za kiitikadi ambazo alikuwa akizitoa kila baada ya muda katika kuijenga nchi yetu ya Tanzania.

Aidha, Mgombea Urais Dkt. Samia amesema hayo yote yalilenga kujenga Taifa imara linalojitegemea na kujenga maendeleo ya watu ambapo amesema Mwl. Nyerere alisisitiza kuwa maendeleo yote yenye maana hayana budi kuwalenga watu na ndicho ambacho katika dira na mipango yote ya maendeleo na hata kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndani yake zimejielekeza kujenga Taifa linalojitegemea lenye uchumi jumuishi na ustawi wa watu.

Dkt. Samia ameyasema hayo leo tarehe 10 Oktoba 2025 mbele ya maelfu ya Wananchi wa Butiama mkoani Mara waliojitokeza katika viwanja vya Mwenge ikiwa ni muendelezo wa mikutano yake ya kampeni za Urais kupitia CCM.

๐™ˆ๐™˜๐™๐™–๐™œ๐™ช๐™š ๐˜ฟ๐™ ๐™ฉ. ๐™Ž๐™–๐™ข๐™ž๐™– ๐™ ๐™ฌ๐™– ๐™ข๐™–๐™š๐™ฃ๐™™๐™š๐™ก๐™š๐™ค ๐™š๐™ฃ๐™™๐™š๐™ก๐™š๐™ซ๐™ช ๐™ฃ๐™– ๐™ ๐™ช๐™š๐™ฃ๐™™๐™š๐™ก๐™š๐™– ๐™ ๐™ช๐™ž๐™ฃ๐™ช๐™– ๐™๐™ฉ๐™ช ๐™ฌ๐™– ๐™ ๐™ž๐™ก๐™– ๐™ˆ๐™ฉ๐™–๐™ฃ๐™ฏ๐™–๐™ฃ๐™ž๐™–