Mke wa rais wa zamani wa Korea Kusini aliyeondolewa madarakani amehukumiwa kifungo cha miezi 20 jela kwa kupokea rushwa kutoka kwa Kanisa la Unification lenye utata.
Hata hivyo, mahakama ilimsafisha Kim Keon Hee mwenye umri wa miaka 52 kwa mashtaka ya kudanganya bei ya hisa na kupokea kura za maoni bila malipo kutoka kwa dalali wa kisiasa kabla ya uchaguzi wa rais wa 2022, ambao mumewe Yoon Suk Yeol alishinda.
Yoon tayari amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela kwa kutumia vibaya madaraka na kuzuia haki kuhusiana na jaribio lake la mapinduzi ya kijeshi lililoshindwa mwaka 2024.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Korea Kusini kwa aliyekuwa rais na mkewe kuhukumiwa wakati mmoja.

