Shirikisho la Soka Afrika (CAF) imeorodhesha adhabu walizotoa kwa Morocco na Senegal kufuatia vurugu iliyoshuhudiwa wakati wa fainali ya AFCON 2026.
Mashabiki wengi wa mpira walikuwa na hamu ya kujua hatua zipi zitashukuliwa na shirikisho hilo huku kila upande ukiamini mwenzake alikosea na anafaa kupata adhabu kali zaidi.
CAF limempiga marufuku kocha wa Senegal, Pape Thiaw, michezo mitano na kumtoza faini ya $100,000 kutokana na mwenendo usio wa kispoti baada ya kuwaambia wachezaji wake waondoke uwanjani wakati wa fainali ya Kombe la Mataifa dhidi ya Morocco.
CAF pia ililazimisha shirikisho la soka la Senegal kulipa faini ya $615,000 kutokana na mwenendo wa timu na mashabiki wake, huku wachezaji Iliman Ndiaye na Ismaila Sarr wakifutwa michezo miwili ya CAF kwa mwenendo wa kutojali taratibu dhidi ya refa.
Hata hivyo, ombi la Morocco la kubatilisha matokeo ya mechi baada ya wachezaji wa Senegal kuondoka uwanjani, jambo lililosababisha kucheleweshwa kwa dakika 14, lilitupiliwa mbali na Kamati ya Nidhamu ya CAF.
Wenyeji Morocco pia walitakiwa kulipa faini jumla ya $315,000 kutokana na mwenendo wa wavulana wa mipira (ball boys) wakati wa mechi, mwenendo wa wachezaji na wafanyakazi wao katika eneo la VAR, pamoja na matumizi ya mwangaza leza na mashabiki.
Kapteni wa Morocco, Achraf Hakimi (michezo miwili ya CAF, mojawapo ikisimamishwa kwa mwaka mmoja) na Ismael Saibari (michezo mitatu ya CAF), walifutwa kwa mwenendo usio wa kispoti baada ya kujaribu kuondoa taulo ya kipa wa Senegal, Edouard Mendy, wakati mvua inanyesha Rabat.
Kocha wa Senegal, Thiaw, aliwaamuru wachezaji wake waondoke uwanjani mwishoni mwa mechi baada ya goli lao kubatilishwa, na dakika chache baadaye Morocco walipatiwa penati, ambayo hatimaye Brahim Diaz aliipoteza.


