Jeshi la Israel limesema jana Jumanne kwamba limetanua operesheni zake kwenye Ukanda wa Gaza siku chache kabla ya ziara ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, mjini Washington.
Wakazi wameripoti mapigano makali siku chache kabla ya ziara ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, mjini Washington.
Operesheni hiyo kubwa inafanywa katikati ya ongezeko la miito ya usitishwaji wa mapigano, miongoni mwao akiwa ni Rais Donald Trump wa Marekani anaetarajiwa kukutana na Netanyahu, wiki ijayo.
Kampeni ya Israel ya kuliangamiza kundi la Hamas imepamba moto na jana Jumanne, shirika linalohusika na ulinzi wa raia la Gaza liliripoti kuwa vikosi vya Israel viliwauwa karibu watu 26.
Na lilipozungumzia shambulizi hilo kubwa ililofanya kaskazini na kusini mwa eneo hilo, lilisema lego ni kudhoofisha kabisa uwezo wa kijeshi wa Hamas.
