Jumla ya watu 18 wamefariki dunia kutokana na kipindi cha baridi kali jijini New York, kwa mujibu wa meya wa jiji hilo.
Tangu mwishoni mwa Januari, jiji hilo limekumbwa na wimbi la baridi kali, likiwemo siku 13 mfululizo ambapo joto lilikuwa nyuzi joto 0°C au chini ya hapo, moja ya vipindi virefu zaidi vya baridi kali kuwahi kushuhudiwa New York katika kipindi cha miaka 60.
Mwishoni mwa wiki, mtu mwingine “alipoteza maisha mitaani katika jiji letu,” alisema Zohran Mamdani siku ya Jumatatu, akiongeza kuwa, “kila maisha yanayopotea ni msiba, na tutaendelea kuyakumbuka familia zao katika mawazo yetu.”
Alisema, “Tumekuwa tukifanya kazi kwa bidii kuhakikisha usalama wa wakazi wa New York, na tutaendelea kufanya hivyo. Kwa sababu joto halitarajiwi kupanda zaidi ya nyuzi 32 za Fahrenheit hadi kesho, na nyuzi 35 si hali ya joto ya kufurahisha hata kidogo.”
Ingawa joto linatarajiwa kupanda kidogo wiki hii, bado lipo chini ya wastani.
Mamdani aliwahimiza wakazi “kuendelea kuwa salama, kukaa ndani ya nyumba inapowezekana, na kujuliana hali kila mmoja.”
Shirika la Usimamizi wa Dharura la Jiji la New York (NYC Emergency Management) limesema kuwa baada ya siku kadhaa za baridi kali na theluji, hatari kubwa za kiusalama bado zipo katika maeneo mengi ya jiji.
Shirika hilo limeonya kuwa theluji na barafu vinavyoyeyuka vinaweza kudondoka kutoka juu ya majengo bila onyo, na kwamba barabara na njia za wasio tunia magari zinaweza kuganda tena wakati wa usiku.

