Category: Kimataifa
Waandishi wa habari watano Gaza wauawa
Kituo cha Televisheni cha Palestina kimesema waandishi wa habari watano kutoka kituo hicho wameuawa katika shambulizi la Israeli katika Ukanda wa Gaza katikati. Walikuwa katika gari la Quds Today lililokuwa limeegeshwa nje ya hospitali ya al-Awda, ambapo mke wa mmoja…
Chombo cha anga za juu cha NASA chajaribu kuweka historia kwa kuwa karibu zaidi na jua
Chombo hicho cha Parker Solar Probe kilisafiri katika angahewa ya nje ya nyota yetu, kikistahimili joto na mionzi mikali. Hakitakuwa na mawasiliano yoyote kwa siku kadhaa wakati huu wa joto kali na wanasayansi watakuwa wakisubiri ishara, inayotarajiwa tarehe 27 Desemba,…
Aliyekuwa rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton alazwa hospitalini
Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton amelazwa hospitalini baada ya kupata homa, kwa mujibu wa msemaji wa chama cha Democrat. “Anasalia katika hali nzuri na anathamini sana utunzaji bora anaopokea,” Angel Ureña aliandika kwenye X, iliyokuwa Twitter. Alisema Clinton…
Watu 38 wafariki Congo, wengine wapotea
Watu 38 wamethibitishwa kufariki dunia na wengine zaidi ya 100 kupotea baada ya Feri iliyokuwa imejaa watu kupinduka kwenye mto Busira Kaskazini – Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo. Katika ajali hiyo ya Feri ambayo ilibeba watu waliokuwa wakirejea…
Trump kuwashughulikia waliobadili jinsia
Rais mteule wa Marekani Donald Trump amepanga kuwashughulikia watu waliobadili jinsia zao nchini Marekani siku ya kwanza atakapoingia madarakani. Kauli hiyo ameitoa wakati Warepublican wakiendelea na juhudi zao za kupinga haki za watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja LGBTQ katika…
Watu 94 wamekufa kufuatia kimbunga Chido
Shirika la kukabiliana na majanga nchini Msumbiji limesema kuwa mpaka sasa idadi ya vifo vilivyotokana na kimbunga Chido vimefikia 94. Wiki moja sasa tangu Kimbunga Chido kutokea na kuishambulia pwani ya Msumbiji na kuathiri maeneo mengi ikiwemo visiwa vya Mayotte….