JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Chadema vaa miwani muone CCM walipoangukia

Wiki iliyopita Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemaliza mkutano wake wa Nane. Katika mkutano huu kimemchagua Mwenyekiti, Rais Jakaya Kikwete Makamu Mwenyekiti Bara, Philip Mangula na wa Visiwani, Dk. Ali Mohamed Shein, huku Wilson Mukama aliyeingia madarakani kwa kuwapiga fitina viongozi waliomtangulia akienguliwa wadhifa huo alioutumikia kwa miezi 17 tu, na ukatibu Mkuu wa CCM ukatua kwa Abdulrahman Kinana.

Na sisi tuchague makamishna wa polisi

ALHAMISI ya wiki iliyopita shule za msingi zilifungwa, watoto wakabaki majumbani na wazazi wao. Kwenye shule zao na katika vituo vingine mbalimbali, kulikuwa na kazi kubwa ya kisasa ya kuchagua makamishna wa polisi na uhalifu.

Yah: Naikumbuka TBC ya kweli

 

Wanangu, naamini hamjambo baada ya kupumzika nyumbani na kutafakari maisha yenu ya miaka ijayo na hatima ya kizazi chenu cha dotcom. Sina hakika miaka michache ijayo baada ya dotcom kuzeeka, sijui kutakuwa na kizazi gani?

Wasemavyo wananchi juu ya ombaomba ya Tanzania

Wiki iliyopita, kwenye safu hii, niliandika makala kuhusu Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kupokea msaada dhalili wa ambulance moja kutoka kwa “Watu wa Marekani”.

Mashabiki sasa wageukia Chalenji

Mashabiki wa soka sasa wamegeukia michuano ya Kombe la Chalenji, itakayoanza kutimua vumbi kwenye Uwanja wa Namboole, Kampala nchini Uganda, Jumamosi wiki hii.

CCM na urais 2015: Tujadili aina za wagombea

Mwaka 2015 si mbali, na kwa mara nyingine tena Watanzania tutapata fursa ya kutumia haki yetu ya kikatiba kumchagua mtu mmoja, ambaye tunaamini kwamba ndiye atakayefaa kutuongoza kama Taifa, katika hiki kipindi kigumu cha uchumi kinachotuathiri kwa miaka zaidi ya 50 sasa.