Category: MCHANGANYIKO
JK usizungumzie usalama wa nchi nyingine
Mheshimiwa Rais, awali ya yote hongera kwa hotuba yako ya mwisho wa mwezi maana ilijaa lugha tamu ya kidiplomasia inayoonesha namna ulivyo muungwana na usiyependa ugomvi au migogoro na nchi majirani zetu.
NUKUU ZA WIKI
Mwalimu Nyerere: Tuendeleze
demokrasia tupate maendeleo
“Jambo kubwa kwa maendeleo ya nchi yetu ni kuendeleza demokrasia yenyewe na siyo muundo unaoiendesha. Jambo hili litakapoletwa ili liamuliwe na mkutano wa Chama, hoja zitakazoongoza uamuzi huo lazima ziwe na uhusiano na hali halisi na mahitaji ya Tanzania ya wakati huo.”
Haya ni maneno ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
KELVIN CHRISTOPHER ‘KIBA GITA’:
Prodyuza anayetamani kumiliki kituo cha redio
Imekuwa jambo la kawaida kwa vijana wengi kukaa vijiweni, kwa kisingizio kuwa Serikali imeshindwa kuwapatia ajira.
FC Lupopo yasifu wachezaji wa Tanzania
*Huenda Kaseja akasajiliwa huko
Katika hali inayoonesha kuwa wanandiga wa Kitanzania wanaosakata kabumbu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wanakubalika, Klabu ya Soka ya FC Lupopo imesema wachezaji kutoka Tanzania wanapendwa nchini humo kutokana na uwezo wao kisoka.
Tenisi wajihami Afrika Mashariki, Kati
Timu ya Taifa ya Tenisi inayoshiriki mashindano ya Afrika Mashariki na Kati kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15, imeondoka leo kwenda Nairobi, Kenya kushiriki mashindano ikiwa na matumaini ya kushinda.
Kodi ya simu inarejesha ‘Kodi ya Kichwa’
Taifa letu lipo katika mtikisiko mkubwa. Kuna mjadala mkubwa unaoendelea juu ya uanzishwaji wa kodi ya kumiliki simu. Kodi hii inatajwa na wengi kuwa ni kama kodi ya ‘Kichwa’ iliyobatizwa jina la kodi ya maendeleo baada ya Uhuru.