JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

FIKRA YA HEKIMA

Serikali itangaze elimu ya msingi haitolewi bure tena

Elimu ya msingi hapa Tanzania imeendelea kuwagharimu wazazi na walezi fedha nyingi, licha ya Serikali kutangaza kuwa inatolewa bure (bila malipo yoyote).

Cameron na vita ngumu ya pombe

Siasa ni mchezo mchafu, kweli wana JAMHURI sasa naamini. Utata wa siasa hauna cha nchi kubwa wala ndogo, maana nchi kubwa kama Marekani au Uingereza zinaweza kuamua siasa, wakakaribia kugawanyika nusu kwa nusu. Uingereza walipopiga kura mara ya mwisho, walishindwa kuchagua chama kimoja kikae madarakani, kwa sababu wabunge waligawanyika.

Sitta anatuchezesha makidamakida EAC

Wiki iliyopita nilisikia malumbano kati ya Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, na wabunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania. Wabunge kutoka Tanzania wakiongozwa na Shy-Rose Bhanji wanasema Serikali kupitia wizara hiyo haiwapi mwongozo wa nini wanapaswa kufanya.

Wanasiasa waepuke rafu kuelekea Uchaguzi Mkuu

Waingereza wanasema ‘Politics is a science.’ Tafsiri rahisi ya maneno haya ni kwamba siasa ni taaluma. Ni vizuri Watanzania tukalifahamu na kulizingatia hili. Katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika nchini mwaka 2015, kumekuwapo na viashiria vya rafu za kisiasa.

Airtel Tanzania sasa kwachafuka

Wafanyakazi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Airtel Tanzania wametangaza mgogoro na mwajiri wao, wakidai haki ya kuachishwa kazi. Wafanyakazi wanaohusika katika mgogoro huo ni 179 kutoka katika Idara ya Huduma kwa Wateja walioajiriwa kati ya mwaka 2001 na mwaka 2011.

Pole sana kaka Absalom Kibanda

Ninahuzunika juu yako kaka yangu Absalom Kibanda. Moyo wangu umejaa uchungu. Kibanda wamekutenda vibaya, wamekuteka, wamekushambulia na kukujeruhi vibaya! Wamekusababishia kilema.